Friday, July 8, 2011

Mambo yanayohusu usajili

Arsenal


Arsenal wanamtaka winga anayeuzwa kwa £15 na Valencia Juan Mata ili acheze na Samir Nasri. (Daily Mirror)


Southampton wameichekea nje ofa ya Arsenal £6m ili kumpata winga Alex Oxlade-Chamberlain. (
Daily Star)


Barcelona watawatoa mabeki wake Maxwell au Eric Abidal ili kumpata kiurahisi Cesc Fabregas. (
Metro)





Chelsea wanamkimbizia kipa wa Genk anayedaiwa kuuzwa kiasi cha pauni millioni 9 Thibaut Courtois kama mrithi wa Petr Cech. (The Sun)




West Ham wanaandaa kitita cha £7.5 million ili kuwasajili Joe Cole and Paul Konchesky . (
Caught Offside)




Patrick Vieira yuko tayari kumshushua kocha wake wa zamani Arsene Wenger kwa kuchukua jukumu la kuwa kwenye bechi la ufundi wa Manchester City (
Goal.com)


Aston Villa wanatumaini kumpata Shay Given kwa £4 million kutoka Man City. (
The Sun)


----------------------------------------------------------------
Manchester United


United wako tayari kutoa ofa kati ya £10-12 million, pamoja na wachezaji wawili ili kumpata kiungo Luka Modric. (
Caught Offside)


Kocha wa Leicester Sven-Goran Eriksson anampango wa kumsaini Owen Hargreaves. (
The Sun)


Sunderland wamepooza kidogo katika kumsajili kiungo Darron Gibson. (
Northern Echo)