Wednesday, December 22, 2010

HODGSON:TULIENI KWANZA

Roy Hodgson amesisitiza kwamba mashabaki wasijawe na hasira sana na wasubiri Januari itakapofika aweze kuwasajili wachezaji na Liverpool itarudi kama kawaida.
Baada ya Liverpool kumaliza msimu uliopita ikiwa namba saba chini ya kocha Rafael Benitez, Hodgson aliajiriwa na mpaka sasa ameshafungwa michezo minane.Kocha huyo ambaye alikuwa kocha Fulham amesema kwamba atawasajili wachezaji wakubwa ili kikosi chake kiimarike vizuri zaidi na ameshahusishwa na mipango ya kuwasajili wachezaji kama Ashley Young, Johan Elmander na Gary Cahill.

"Klabu nyingi zimeendeshwa chini ya uongozi mzuri lakini kocha akiingia kwenye kuwasajili wachezaji, anaweza akawasajili wachezaji lakini inatokea kwamba mchezaji uliyemnunua hakuwa anayetakiwa kuwapo pale kwaio nawaomba mashabiki kwamba watulie itachukuwa mda lakini Liverpool itakuwa Liverpool ya zamani."


"Lakini tunachotakiwa kujua unaposajili wachezaji kuna wachezaji wadogo ambao wakikuzwa watacheza mpira vizuri zaidi. Kama hapa Liverpool sasa tunao wachezaji wadogo kama (Jonjo) Shelvey na (Martin) Kelly na ndio maana ukienda kusajili wachezaji unatakiwa kuwafikiria wachezaji wadogo kama hawa kwamba Je, atapata nafasi ya kucheza na kukuzwa na kuwa staa wa baadaye au unaangamiza kiwango chake kwa kuwaleta wachezaji wakubwa?.